Uchaguzi Marekani 2020: Kanye West atangaza kuwania urais wa Marekani

Mtoto wa Kanye West na Kim Kardashian 'North West' kutambulishwa ...
Kanye West amekuwa akizungumzia suala la kuwania urais nchini Marekani miaka kadhaa nyuma

Kanye West amesema anawania urais wa Marekani. Haifahamiki kama mwanamuziki huyo amemaanisha kweli kile alichokisema, au hiyo ni njia tu ya kutafuta kuzungumziwa tu ifahamikavyo na wengi (Kiki) limeeleza shirika la habari la Bloomberg.

Ujumbe wa Kanye uliowekwa kwenye mtandao wa Twitter siku ya Jumamosi usiku ulisambaa sana mitandaoni, huku ukirudiwa kuchapishwa mara 100,000 ndani ya kipindi cha saa nne. West ana wafuasi milioni 29.4 kwenye mtandao wa Twitter. 'Kanye' kwa haraka sana akawa ndiye anayezungumziwa zaidi kwenye mtandao huo nchini Marekani.

''Lazima sasa tutambue ahadi ya Marekani kwa kumuamini Mungu, kuunganisha maono yetu na kujenga mustakabali wetu,'' West aliandika akinukuliwa na gazeti la The Guardian.
Kanye West adai watumwa walijitakia - Mwananchi

ye
 @kanye west
We must now realize the promise of America by trusting God, unifying our vision and building our future. I am running for president of the United States 🇺🇸! #2020VISION
3:38 AM · Jul 5, 2020
1.2M
408.7K people are Tweeting about this

Ikiwa imebaki miezi minne kabla ya kura za tarehe 3 mwezi Novemba, haijabainika kama tweet ya West ingefaa zaidi katika siku ya wajinga duniani ya mwezi Aprili kuliko siku ya maadhimisho ya uhuru wa Marekani.

Kama West alichokisema kilikuwa si cha masihara, basi kuna mlolongo mrefu wa vihunzi katika kuelekea azma hiyo, ikiwemo kuanza kampeni tangu awali mwezi Julai mwaka huu wa uchaguzi. Atahitaji kufuzu katika majimbo 50 na pia kujenga taasisi ya kisiasa kuanzia mwanzo bila usaidizi.

Kwa sasa, West hajaonekana kujaza fomu za tume ya uchaguzi nchini humo kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo ya juu, kwa mujibu wa Bloomberg baada ya kupitia data za tume hiyo FEC,
Kanye West azuia mkanda wa ngono sokoni - Mtanzania
West, 43, amezungumzia suala la kuwania urais miaka kadhaa nyuma, na mwaka jana aliiambia hadhira yake kuwa atawania urais mwaka 2014. Yeye na mkewe, Kim Kardshian West, wamefanya kazi na rais Donald Trump mara kadhaa ikiwemo wakati wa shughuli za kuwafungulia wafungwa.

West na mkewe walishawahi kumtembelea Trump kujadili mabadiliko katika magereza mwaka 2018, baada ya mkutano huo West alimsifu Trump akisema amemfanya kujihisi shujaa, akamkumbatia na kukiri: ''Ninampenda huyu mtu.''

Trump aliulizwa kama West anaweza kuwa rais siku moja ,Trump alijibu: ''Sana tu anaweza kuwa.''


Comments