Wezi Wavamia Ofisi za TRA Na Kuiba Nyaraka za Kodi, Laptop Moja


Watu wasiojulikana ambao idadi yao haijulikani wamevamia ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kodi wa Kahama, Shinyanga na kuondoka na kompyuta mpakato moja na baadhi ya nyaraka za kodi pamoja na Sh2 milioni baada ya kuwafunga kamba walinzi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Richard Abwao alisema jana kuwa watu hao walivamia ofisi hizo usiku wa kuamkia jana na kwamba uchunguzi unaendelea kubaini waliohusika na sababu za kufanya hivyo kama ni kuiba fedha au nyaraka za ofisi.

Alisema watu hao baada ya kuwafunga kamba walinzi walivunja dirisha la nyuma na kisha kuingia ndani na kupora vitu hivyo na kwamba kwa sasa walinzi hao wanashikiliwa pamoja na baadhi ya maofisa wa mamlaka hiyo ili kusaidia uchunguzi wa polisi.



Comments