Simba SC waing’arisha Tanzania nchini Kenya, watinga nusu fainali michuano ya SportPesa Super Cup

Klabu ya Simba SC imefanikiwa kutinga nusu fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup kwa kuichabanga goli 3-2 klabu ya Kariobangi Sharks FC kwa njia ya changamoto ya mikwaju ya penati baada ya timu hizo kutoka 0-0 ndani ya dakika 90 .

Simba SC inakuwa klabu ya kwanza kutoka Tanzania kufuzu kwenye michuano hiyo hii ni baada ya watani zao wa jadi klabu ya Yanga kutolewa kwenye michuano hiyo siku ya jana.

Simba watakutana na wababe waliowatoa Yanga, Kakamega HomeBoyz FC siku ya Alhamisi Juni 07, 2018.

Comments