TUZO YA WEMA SEPETU YAZUA MAZITO


Image result for WEMA SEPETU AKIPOKEA TUZO images
DAR ES SALAAM: BAADA ya wiki iliyopita staa wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu kushinda tuzo mbili katika hafla ya Tuzo za Sinema Zetu zilizofanyika ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, mambo yamekuwa mambo kutokana na baadhi ya wadau pamoja na mastaa wenzake kupinga ushindi wake huo.

Image result for WEMA SEPETU AKIPOKEA TUZO images
 Mara baada ya Wema kukabidhiwa Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike na ile ya Msanii Bora Chaguo la Watazamaji hapo ndipo minong’ono ilianza ambapo iliendelea pia katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba mrembo huyo hakustahili kwani wapo wasanii wengi wa kike ambao wanajua kuigiza kuliko mwanadada huyo.

 “Kiukweli Wema hakustahili kupata hiyo tuzo maana wasanii kama Riyama Ally ndiyo wanastahili maana wanajua kuigiza jamani lakini nashangaa amepewa yeye inawezekana watu wanavutiwa tu na umaarufu wake na siyo kazi yake maana hata filamu zenyewe anacheza mara chache sana siyo kama wengine,” alisema mmoja wa mastaa ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini.

Akizungumza na Amani, msanii wa filamu Kulwa Kikumba ‘Dude’ alisema Wema amepata ushindi kwasababu kura alikuwa akipigiwa na mashabiki ambao wengi hupiga kutokana na jinsi wanavyomuona au kumsikia mtu kwa muonekano wa nje lakini hawaangalii kazi zao husika.

 “Mpoki aliwahi kuibuka mwimbaji bora wa nyimbo za asili Kili Music Award akawashinda manguli wa muziki huo kama Wanne Star na Mrisho Mpoto, hiyo ndiyo faida ya kura za mashabiki, sasa hapo ndipo kwenye tatizo. Sikatai Wema kushinda lakini tatizo linakuja, waandaaji wa tuzo wa nje, wanaweza kumsikia Wema ameshinda nchini, wakimpeleka kule, atafeli maana ni ukweli ulio wazi kwamba Wema hawezi kuwazidi waigizaji wengine kama Riyama,” alisema Dude.

 Kwa upande wake Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ yeye alihoji mastaa wengine kama JB, Rich, Aunt Ezekiel, Shamsa Ford, Duma, Ray na wengine wengi walikuwa wapi hawakuonekana kwenye tuzo hizo.

“Nitaongea nilichokiona jana kwenye tuzo ,kwani Ray, JB, Rich, Aunt Ezekiel, Shamsa Fodi, Duma, Weru, Hemedi, Tausi Mndengela, Mainda, Johari, Uwoya, Marian Ismail, Batuli na wengine wanaofanya vizuri wapo wapi?” alihoji Steve kuonesha hakubaliani na ushindi wa Wema.

Comments