Davido kuachia kitu kipya Ijumaa hii

Baada ya kufanya vizuri na wimbo wa ‘If’ Davido amepanga kuachia kazi yake mpya Ijumaa hii.

Muimbaji huyo wa Nigeria amethibitisha kuachia video yake mpya ya wimbo uitwao ‘Fall’ siku hiyo iliyotajwa hapo juu ambapo video hiyo imeongozwa na Daps.

“FALL 02/06/17,” ameandika msanii huyo katika mtandao wake wa Instagram.
Wakati huo huo Davido ni miongoni mwa wasanii watano kutoka Afrika wanaowania tuzo ya BET katika kipengele cha Best International Act: Africa ambapo anachuana na Wizkid, Tekno, Mr Eazi (wote kutoka Nigeria), Stonebwoy (Ghana), na Nasty C, Babes Wodumo na AKA (wote kutoka Afrika Kusini).

Comments