Vipuli vya almasi vyauzwa $58m katika mnada

Vipuli vya Apollo na Artemis ambavyo mauzo yake yalivunja rekodi katika mnada
Vipuli vya Apollo na Artemis ambavyo mauzo yake yalivunja rekodi katika mnada
Vipuli viwili vya almasi, vimevunja rekodi ya dunia kwa kuuzwa kwa kiwango kikubwa zaidi cha pesa, cha takriban dola milioni 58, katika soko la mnada nchini Uswizi.
Vipuli hivyo viko sawa, lakini kimoja kina rangi ya waridi na chengine ni cha buluu.
Viliuzwa tofauti tofauti lakini vikanunuliwa na mnunuzi mmoja.
Kulikuwa na wasiwasi kwamba vipuli hivyo, vinavyojulikana kama Apollo na Artemis havitakuwa pamoja baada ya kupigwa mnada mjini Geneva.
Viliuzwa tofauti kwa sababu almasi za buluu ni nadra ukilinganisha na zile za rangi ra waridi.
Hata ijapkuwa ziliuzwa tofauti lakini vitasalia kuwa pamoja baada ya kupata mnunuzi mmoja.
Alamasi ya Apollo yenye rangi ya buluu iliuzwa kwa takriban dola milioni 42 huku Artemis yenye rangi ya waridi ikiuzwa kwa dola milioni 15.5

Comments