Trump 'kufanya kila awezalo' kuidhinisha amani mashariki ya kati

Donald Trump and Mahmoud Abbas - 23 May
mwisho ya ziara ya kiongozi huyo mashariki ya kati.
Raia katika maeneo ya Gaza na ukingo uliokaliwa wa magharibi kupinga ziara hiyo na kuunga mkono wafungwa wa Palestina walioko katika magereza ya Israel waliogoma kula.
Jumatatu Trump alisema amekuja "kuhakikisha uhusiano usiovunjika" kati ya Marekani na Israel na kuna "nafasi iliyo adimu ya kuidhinisha usalama utulivu na amani kwa eneo hilo".
Aliwasili Tel Aviv kutoka Saudi Arabia ambako katika mkutano Jumapili aliwaomba viongozi wa kiislamu na kiarabu kuwatokomeza waislamu wenye itikadi kali.
Picha za kumkaribisha Trump Bethlehem Picha za kumkaribisha Trump Bethlehem                
Trump amesema amekuja Bethlehem 'kwa matumaini', ni eneo ambako amekutana na Bwana Abbas Jumanne asubuhi.
Ameongeza kuwa "anashukuru" kwamba Abbas alihudhuria mkutano huko Riyadh na "kuahidi kuchukua hatua madhubuti zinazo hitajika kukabiliana na ugaidi na fikra zake za chuki".
"Amani haiwezi kuweko katika eneo ambapo ghasia zinaendekezwa, kufadhiliwa na pia kutuzwa," aliongeza, inavyoonekana ni kama anataja malipo yaliotolewa na utawala wa Palestina kwa familia za wafungwa wa Palestina na waliouawa katika mzozo na Israel.
Msafara wa rais ulipita katika eneo lililozusha mzozo la ukuta uliojengwa na Israel katika ukingo wa magharibi Msafara wa rais ulipita katika eneo lililozusha mzozo la ukuta uliojengwa na Israel katika ukingo wa magharibi                
Abbas amekaribisha azimio la Trump analolitaja kuwa la "ukarimu na linalowezekana".
Baadaye Jumanne Trump alirudi Jerusalem. alilitembelea eneo la kumbu kumbu la mauaji ya kimbari la Yad Vashem.

Comments