NUNDU YA HARMORAPA KUDONDOKA LEO

Msanii wa muziki bongo Harmorapa anatarajia kuachia ngoma yake mpya siku ya leo iitwayo Nundu aliofanya na producer Ronei.

Harmo, wa kiboko ya mabisho, amesema kuwa nyimbo hiyo itazima ngoma zote zilizotoka kutokana na ubora wake na ukali wa ngoma hiyo ambayo imeshirikisha wasanii watatu akiwepo yeye, mkongwe katika muziki wa Crank Cpwaa pamoja na msanii mpya bongo aitwaye Ronei.

“Vijana wadogo ila tuna balaa, nipo na fundi wa muziki kutoka SGS wakuitwa Ronei, leo ‘Nundu’ inatikisa jiji na kuzima ngoma zote zilizoachiwa hivi karibuni”amesema Harmorapa.
Hii itakuwa ngoma ya tatu kwa msanii huyo kumuweka katika ramani ya muziki tangu alipoanza kujulikana na usigawe pasi ,kisha kiboko ya mabisho na sasa Nundu.

Comments