Majeshi yanayoungwa mkono na Marekani yakaribia ngome ya IS Syria

Raqqa ni miongoni mwa sehemu zinazoshikiliwa na IS Syria
Raqqa ni miongoni mwa sehemu zinazoshikiliwa na IS Syria
               
Majeshi yanayoungwa mkono na Marekani nchini Syria yamesema kuwa yamesonga mbele kwa zaidi ya kilomita nne kuelekea kwenye ngome wanamgambo wa Islamic State iliyopo Raqqa.
Msemaji wa kundi la Kurdish-led Syrian Democratic Forces, SDF, amesema wameweza kuteka vijiji vitano vinavyozunguka eneo la Raqqa tokea siku ya Jumatatu.
SDF wamewataka IS kujisalimisha na kujali familia zao.
Wameongeza kuwa watafanya shambulizi kubwa Raqqa siku za usoni.

Comments