Juventus yatinga fainal

Wachezaji wa klabu ya Itali Juventus wakisheherekea ushindi wao dhidi ya Monaco
Wachezaji wa klabu ya Itali Juventus wakisheherekea ushindi wao dhidi ya Monaco
               
Klabu ya Juventus kwa mara ya pili imefuzu katika fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya baada ya kuishinda Monaco kwa jumla ya mabao.
Wakiwa wanaongoza 2-0 katika awamu ya kwanza ya mechi ,timu hiyo ya Itali iliongeza jumla ya mabao wakati mshambuliaji wao Mario Mandzukic alipofunga .
Dani Alvez aliongeza bao la pili baada ya kipa Danijel Sabusics kuupangua mpira ulioanguka mbele yake.
Kylie Mbappe alifunga krosi iliopigwa katika kimo cha nyoka ya Joao Moutinho ili kufunga bao la kufutia machozi, lakini klabu hiyo ya ligi ya daraja la kwanza haikuweza kufunga zaidi ya bao moja.
Juventus ambao hawajashinda kombe hilo tangu 1996 na waliopoteza katika fainali ya mwaka 2015 dhidi ya Barcelona watakabiliana na Real Madrid au Atletico Madrid katika uwanja wa Cardiff mnamo tarehe 3 mwezi Juni.

Comments