WATU 23 WAFARIKI DUNIA KATIKA AJARI YA MELI ILIYOTOKEA HUKO INDONESSIA

Watu 23 wamefariki dunia Jumapili hii na wengine 17 hawajulikani walipo nchini Indonesia baada ya kuzuka kwa moto kwenye meli iliyokuwa imebeba watu zaidi ya 200.

Waokoaji wakiendelea na zoezi la kuokoa watu kwenye ajali hiyo

Imedaiwa kuwa meli hiyo ilikuwa ikisafiri kuelekea katika kisiwa cha utalii cha Tidung Island kilichopo Mashariki mwa mji wa Jakarta.

Afisa mmoja wa jeshi la polisi wa nchi hiyo, Hendrianto Bachtiar ameiambia CNN kuwa watu 194 wameokolewa kasoro 17 ambao bado hawajaonekana lakini pia wanamshikilia nahodha wa meli hiyo kwa ajili ya kupata maelezo zaidi.

“We have detained the captain of the boat, and are now taking his statement,” amesema Bachtiar

Comments