KUMBE CHUCHU HANSY AJAJIFUNGUA?


Kama wewe ni mpenzi wa movie za kibongo basi naamini kabisa jina la staa Vincent Kigosi a.k.a Ray pamoja na mpenzi wake Chuchu Hans halitokuwa geni masikioni mwako na zaidi kuhusu wao stori za wao kuwa mapenzini.

Hivi karibuni kumeibuka taarifa zaidi kwenye mitandao ya kijamii zikisema kuwa tayari wapenzi hao wamebahatika kupata mtoto wao wa kiume, lakini leo January 13 2016 Ray kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika ujumbe uliosomeka…>>>

‘Kwanza Kabisa Napenda Kumrudishia Sifa Na Utukufu Mungu Baba Muumba Wa Mbingu Na Ardhi Tumepitia Vingi Vikwazo Lakini Yeye Atutiaye Nguvu Aliendelea Kusimama Na Sisi Imara‘ –Ray

‘Asante Sana Mungu Kwa Kuwa Mwema Kwetu Mengi Yalisemwa Juu Yetu Lkn Mungu Baba Umejibu Ulikuwa Mwezi Mmoja Kama Utani Vile Hatimaye Imefika Miezi tisa Na Sasa Kubaki Siku Chache Nakuombea My Lovely Mzungu Mungu Akufanyie Wepesi‘ –Ray

Comments