SEKI:VENGU AJAFA


Kumekuwa na story ambayo imeenea sana mitandao ya kijamii na pia watu wamekuwa wakitumiana PICHA Whatsapp na wengine wameweka pia kwenye kurasa za Instagram na kuandika #RIP picha ya mchekeshaji wa kundi la Orijino Komedi, Joseph Shamba aka Vengu ambaye ni muda mrefu hatujamuona akiigiza pamoja na kundi lake kutokana na kuumwa. 


Taarifa ambayo Clouds FM imeipata baada ya kuwasiliana na Seki pamoja na Joti ni kwamba hakuna ukweli wowote kuhusu taarifa za msanii huyo kufariki.


Kuna taarifa zilizosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa muigizaji wa vichekesho #Vengu kafariki dunia.. Kwa mujibu wa Meneja wake #Seki na muigizaji mwenzake #Joti wamekanusha taarifa hizo na kusema yuko hai..“–@

Comments