ROSE NDAUKA AFANYA KUFURU KATIKA KUSHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA CHEKI YALIYOJIRI

 Usiku wa kuamkia leo ulikuwa ni usiku wa furaha kwa staa wa Filamu Bongo, Rose Ndauka, kwani aliweza kusheherekea siku yake ya kuzaliwa na baadhi ya mastaa wenzake waliyofurika ndani ya Hoteli ya Collossium iliyopo maeneo ya Kamata Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
 Rose Ndauka (kushoto), akimlisha kipande cha keki rafiki yake mpendwa Jack Pentzel, muda mfupi baada ya zoezi la kulishana keki kuanza kwenye sherehe yake ya kuzaliwa iliyofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya Ukumbi wa Collosseum Hoteli Kamata Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Rose akimlisha keki mwigizaji mwenzake Mayasa Mrisho 'Maya'.
 Mwigizaji Jimmy Mafuvu akilishwa keki hiyo na Rose Ndauka.
 Maya akifungua shampeni kama ishara ya upendo kwa Rose Ndauka ambaye alikuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa.
 Rose Ndauka akimnywesha shampeni Jack Pentzel. 
 
Rose (kulia), akivishwa pete ya dhahabu na dada ake ikiwa kama moja ya zawadi yake katika kusrekea siku ya kuzaliwa kwake. 
 
 Jack Pentzel akimmiminia noti Rose Ndauka kama moja ya zawadi yake.



Comments