WEMA SEPETU KUTOA TSH MILLIONI 1 UKIMFANYIA HIKI KITU

 
Beautiful Onyinye, Wema Sepetu.

BEAUTIFUL Onyinye, Wema Sepetu ametangaza dau la shilingi milioni moja kwa yeyote atakayefanikisha kupatikana kwa mbwa wake aitwae Vanila aliyepotea hivi karibuni.Akielezea ishu hiyo, Wema alisema mbwa huyo alikuwa na mwenzake akiishi nao nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar es Salaam ambapo juzikati alikorofishana na mwenzake aitwae Thiona na kuamua kutokomea kusikojulikana.   
 
Mbwa wa Wema Sepetu aitwae Vanila.

 Msanii huyo alisema anaomba yeyote atakayemuona Vanila wake awasiliane naye au atoe taarifa kituo chochote cha polisi kilicho karibu naye na atakabidhiwa pesa zake taslimu.



Comments