RAPPER TYGA AMTOSA MPENZI WAKE NA HIKI NDO CHANZO

tyga
Rapper Tyga amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Blac Chyna kwa muda wa miaka 3 na kupata mtoto wa kiume King Cairo. Blac Chyna aliwai kuwa stripper na video model hivi sasa imeripotiwa kwamba hayupo tena kwenye uhusiano na Tyga.
Chanzo kikubwa cha Tyga kumuacha mwanamke huyo ni story kuhusu Blac Chyna kujihusisha kwenye mapenzi na mpenzi wake zamani anaitwa Fat Trel. Story hizo zinasema kwamba Blac Chyna alikuwa anatumia muda kujiachia na ex lover wake kwenye nyumba ya Tyga huko L.A na mtoto King Cairo akiwa chumba cha pili.
Japokuwa Blac Chyna amekanusha hizo story lakini Tyga hamuhusishi tena kwenye vitu vyake, mfano ameandaa party zaidi ya mbili lakini zote Blac Chyna hakualikwa. Mmoja kati ya hizo Tyga aliandaa birthday pool party ya msichana Kylie Jenner.
chyna

Comments