MENINAH AFUNGUKA KUHUSU UHUSIANO WAKE NA DIAMOND

meninah 
Mwanzoni mwa wiki hii kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii kumesambazwa taarifa za kuhusishwa uhusiano wa kimapenzi kati ya Meninah ambaye ni msanii wa Bongo Fleva na Diamond Platnumz.

Kupitia kipindi cha Leo Tena ambacho kinaendeshwa na Clouds Fm Meninah amekubali kuongelea tuhuma hizi ambazo zimejitokeza ghafla na kusambaa kwenye mitandao hiyo ya kijamii.
Sentensi 5 alizozisema Meninah ni hizi.
1.Sina uhusiano wowote na Diamond Platnumz
2.Mara ya mwisho kuonana nae ilikuwa Dodoma kwenye uzinduzi wa video ya Miaka 50 ya Muungano.
3.Sijawahi kuwasiliana nae hata namba yake ya simu sina kwenye simu yangu.
4.Mimi napenda uhusiano wao kati yake na Wema Sepetu.
5.Nampenda Wema kama dada yangu na namkubali Diamond Platnumz kama msanii mwenzangu.

Comments