KUMBE NUH MZIWANDA NA SHILOLE WAMEACHANA

Nuh-Mziwanda

Siku ya jana haikua nzuri kwa Shilole na Nuh Mziwanda

baada ya kugomabana sana hadi Nuh Mziwanda akaamua

kuchukua vitu vyake na kuhama Kwa Shilole, Gazeti la

Makorokocho imezipata taarifa hizi za motomoto kupitia

kwa mtu

aliyekuepo eneo la tukio aliyedai kuwa yeye alishangaa

kuskia mikikimikiki ndani ya Harrier na baadae milango ya

gari ikafunguliwa wakatokeza wasanii wawili wa bongo flava

ambao ni Shilole na Nuh Mziwanda na walikua

wakirushiana maneno ghafla wakatokeza watu

wengine wakiongozwa na Msanii Chege

Chigunda wakaamulizia ugomvi huo bila Mafanikio

kwani Nuh Mziwanda alikua anamuambia Shilole

amrudishie simu yake lakini Shishi alishindwa kufannya

hivyo kwa madai eti ufunguo upo nyumbani, Kweli? wakati

dakika chache zilizopita walikua ndani ya Gari.

Nilipomtafuta Nuh Mziwanda hakutaka kubisha na akatiririka

A to Z ya sakata hilo, Nuh Mziwanda: Jana Usiku tulialikwa

Chakula Usiku kwa Producer Dibanjo, mitaa ya

Mango Garden Kinondoni, mimi na Shilole tulipofika

pale tukamkuta mwenyeji wetu pamoja na wasanii wengine

Chege, Julio, Dully Sykes na wengine, ikafika muda nikawa

sijiskii vizuri nikamuomba Shishi funguo ya gari ili

nikapumzike kwenye gari, kufika kule nikazikuta simu za

Shilole zikiwa na missed call nyingi pamoja na msg,

nikazikagua na kukuta msg ya mwanaume akimwambia

Shilole "Nimeingia Dar" .... ikabidi nimuite Shilole

na kumkaripia sana Shishi akajitetea kuwa yule si bwana

wake, Nikamwambia sawa mpigie niskie maongezi yenu,

lakini Shishi alipompigia sikuelewa maongezi ndo

nikamzaba kibao cha nguvu na Shishi akajibu mapigo kwa

kuning'ata mwilini pamoja na kidole changu

kimevimba mpaka wakati huu, watu wakajaa eneo la

tukio hadi kina Chege wakafika na kuanza kuamulizia

kupigana lakini mwisho wa siku Shilole alikua amenipokonya

simu yangu nilipomuomba akakataa kuirudisha na kuondoka  eneo la tukio,

Ikabidi na mimi nisepe kwenda Nyumbani kwa Shilole

ambako nilikua naishi nae ila nia yangu ilikua ni kwenda

kuchukua vitu vyangu ili nihame nyumba ile, njiani karibu

nafika nikakutana na vibaka wakaniibia mpaka viatu,

nikaendelea na safari lakini nilipofika pale kumbe Shishi

alikua amempigia simu Dada wa Kazi asinifungulie mlango,

ikabidi nikae hapo nje weeee mida mida Shilole akafika na

kupitiliza ndani akajifungia mimi nikiwa nje, asubuhi

wakajisahau na kuacha mlango wazi ndipo nilipopata

upenyo nikaingia na kuchukua laptop, guiter pamoja na

nguo vyote vyangu na kumwachia nyumba yake.

Comments